Psalms 59:5-10
5 aEe Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli!
Zinduka uyaadhibu mataifa yote,
usionyeshe huruma kwa wasaliti.
6 bHurudi wakati wa jioni,
wakibweka kama mbwa,
wakiuzurura mji.
7 cTazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao,
hutema upanga kutoka midomo yao,
nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
8 dLakini wewe, Bwana, uwacheke;
unayadharau mataifa hayo yote.
9 eEe nguvu yangu, ninakutazama wewe,
wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
10 Mungu wangu unipendaye.
Mungu atanitangulia,
naye atanifanya niwachekelee
wale wanaonisingizia.
Copyright information for
SwhKC